
SIKU moja baada ya mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba kutangaza nia yake ya kugombea urais wa Muungano, katibu wake, Maalim Seif Sharif Hamad ametangaza rasmi nia ya kugombea urais wa Zanzibar.
Maalim Seif, ambaye aliwahi kuwa Waziri Kiongozi wakati wa utawala wa Aboud Jumbe, atakuwa akiwania urais wa Zanzibar kwa mara ya nne tangu mfumo wa siasa za vyama vingi urejeshwe.
Maalim Seif, ambaye alikuwa akitarajiwa kugombea tena na ambaye hatarajiwi kuwa na mpinzani, amesema anasubiri muda wa kuchukua fomu utangazwe kwa mujibu wa chama chake ili achukue.
No comments:
Post a Comment